J-FILM 4 LIFE ADVERT
FILAMU MPYA YA CHOCOLATE INAKUJIA HIVI KARIBUNI. CHOCOLATE FILM COMING SOON!!
FILAMU MPYA YA HOUSE MAID KUINGIA SOKONI JULAI 2012
FILAMU KALI YA KITANZANIA-RUDE ILIYOSHEHENI WASANII WAKALI. FILAMU IMEANDALIWA NA JENNIFER KYAKA
Tuesday, September 18, 2012
WASEMAVYO WADAU WANGU: "ODAMA APATA SHAVU UINGEREZA NA MALAYSIA"
Jennifer Kyaka ‘Odama’.
SISTADUU wa tasnia ya filamu za Kibongo, Jennifer Kyaka ‘Odama’ amekula shavu la kufanya ziara ya kikazi nchini Malaysia na Uingereza.
Rafiki wa karibu wa Odama aliiambia Bongowood kuwa staa huyo aliondoka nchini hivi karibuni baada ya kupata shavu kutoka kwa maprodyuza wa Nigeria ambapo atafanya nao ziara ya kikazi katika nchi hizo mbili kisha atarejea Bongo kuleta maujuzi ya kuendeleza tasnia hiyo.
BELLA:'NICHEZEWA NYWELE NA LUTEN KALAMA NAKUA TAABANI'
Bella anayewakilisha Kundi la Bongo Fleva la Scorpion Girls alitiririka kuwa anapokuwa kwenye sita kwa sita huwa hana ujanja pale mpenzi wake, mwanamuziki Kalama Masoud ‘Luten’ anapomchezea nywele kichwani na ‘chakula ya mtoto’ kifuani.
“Sijui huwa najisikiaje lakini nashangaa tu mizuka inanipanda, inakuwa… kaazi kwelikweli!,” alifunguka Bella.
Kuhusu kuhusishwa na skendo za kutoka na wanaume tofauti, Bella alichomoa na kudai kuwa kazi yake ya sanaa ndiyo inayomkutanisha na wadau tofauti na si kila mwanaume atakayetajwa then anavunja naye amri ya sita.
SHILOLE AHOFIA KUPORWA BWANA NA MASHOSTI ZAKE
STAA wa filamu na muziki wa mduara, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ ameiambia Bongowood kuwa anaogopa kumtambulisha kwa mashosti zake bwana’ke aliyenaye kwa sasa akihofia kuporwa.
Shilole anayedaiwa kunasa kwenye penzi la mtangazaji (jina tunalo), alisema kuwa anaogopa kumweka hadharani kwani kuna baadhi ya wasichana wa mjini wakishamjua mwanaume wa mtu, huwa wanamnyemelea na kumnasa kirahisi, jambo ambalo hataki limtokee.SHILOLE AHOFIA KUPORWA BWANA NA MASHOSTI ZAKE
STAA wa filamu na muziki wa mduara, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ ameiambia Bongowood kuwa anaogopa kumtambulisha kwa mashosti zake bwana’ke aliyenaye kwa sasa akihofia kuporwa.
Shilole anayedaiwa kunasa kwenye penzi la mtangazaji (jina tunalo), alisema kuwa anaogopa kumweka hadharani kwani kuna baadhi ya wasichana wa mjini wakishamjua mwanaume wa mtu, huwa wanamnyemelea na kumnasa kirahisi, jambo ambalo hataki limtokee.SHILOLE AHOFIA KUPORWA BWANA NA MASHOSTI ZAKE
STAA wa filamu na muziki wa mduara, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ ameiambia Bongowood kuwa anaogopa kumtambulisha kwa mashosti zake bwana’ke aliyenaye kwa sasa akihofia kuporwa.
Shilole anayedaiwa kunasa kwenye penzi la mtangazaji (jina tunalo), alisema kuwa anaogopa kumweka hadharani kwani kuna baadhi ya wasichana wa mjini wakishamjua mwanaume wa mtu, huwa wanamnyemelea na kumnasa kirahisi, jambo ambalo hataki limtokee.ROSE NDAUKA:'FILAMU ZA KIBONGO HAZIPENDWI KIMATAIFA'
Rose Donatus Ndauka.
SURA ya mauzo katika sinema za Kibongo, Rose Donatus Ndauka amekiri kwenye Bongowood kuwa filamu nyingi za Kibongo hazipenyi kwenye soko la kimataifa kutokana na ukweli kwamba waigizaji wengi hawana elimu ya sanaa hiyo hivyo ni ziro kabisa.
Rose alisema kwa upande wake analitambua hilo ndiyo maana yupo kwenye hatua za mwisho za kujiunga na chuo cha sanaa ambacho hakukitaja ili kuongeza elimu katika sanaa hiyo.
ROSE NDAUKA:'FILAMU ZA KIBONGO HAZIPENDWI KIMATAIFA'
Rose Donatus Ndauka.
SURA ya mauzo katika sinema za Kibongo, Rose Donatus Ndauka amekiri kwenye Bongowood kuwa filamu nyingi za Kibongo hazipenyi kwenye soko la kimataifa kutokana na ukweli kwamba waigizaji wengi hawana elimu ya sanaa hiyo hivyo ni ziro kabisa.
Rose alisema kwa upande wake analitambua hilo ndiyo maana yupo kwenye hatua za mwisho za kujiunga na chuo cha sanaa ambacho hakukitaja ili kuongeza elimu katika sanaa hiyo.
DIAMOND Afunguka: "HUU NDIO UKWELI KUHUSIANA NA MAHUSIANO YANGU MIMI NA WEMA SEPETU"
Baada ya msanii anae-make headlines za kutosha Diamond Platnumz weekend iliyopita kukanusha habari zilizochapishwa na gazeti la Risasi kuwa ana mahusiano mapya ya kimapenzi na binti kutoka Kenya, sasa amefunguka tena kuhusiana na yeye na Wema Sepetu kupitia website yake.
Soma alichokiandika:
"Najua watu wengi sana mnapenda Couple hii na furaha yenu ni kutuona wawili sisi tukiwa kwenye Mahusiano ya kimapenzi.... na mmekua mkifurahi sana na story za hapa na pale mkiskia kua wawili sisi tumekua pamoja na hata pindi mkituona tuko pamoja pia Mmekua mkishangilia na kufurahi...
bt ukweli ni kwamba Mimi na Wema hivi sasa si Wapenzi tumekua ni kama Dada na Kaka ama marafki tu wa kawaida ambao tunashirikiana katika kazi mbalimbali za sanaa na za n'nje ya sanaa, katika harakati za kujenga Taifa Letu... Pia ni vizuri ningependa mfahamu kwamba Wema ana Mpenzi wake ambae namfaham na tunaheshimiana kama mtu na Shemeji yake........So das' de Truth abt me and Her!... and Get ready! kwa kazi tofautitofauti ambazo soon zitadondoka....".
Habari ndio hiyo!
J-FILM 4 LIFE INAKUPA POLE STEVE NYERERE KWA KUFIWA NA MWANAO
Mchekeshaji aliyejizolea umaarufu nchini kwa kumuigiliza hayati Baba wa Taifa, Steve ‘Nyerere’ Mangere amefiwa na mtoto wake.
Kwa mujibu wa majirani zake, mtoto huyo wa kiume amefariki baada ya kuishi kwa siku mbili tangu azaliwe.
Huyo ni mtoto wa pili kufariki kwenye familia ya Steve na mke wake aitwaye Zawadi.
“Sababu za kifo cha kwanza sijakijua, ila huyu wanasema atakuwa alivutwa wakati wa kuzaliwa, maana mtoto alikuwa mkubwa mno, sijajua ni kilo ngapi,” kilisema chanzo hicho kilicho jirani na Steve.
“Wa kwanza alifariki, wa pili yupo na huyu wa tatu amefariki.”
Kwa mujibu wa chanzo hicho, mazishi ya mtoto huyo yalifanyika jana.
Bongo5 inampa pole Steve kwa msiba huo.
MUONEKANO MPYA WA MUINGIZAJI ELIZABETH MICHAEL 'LULU'
Muigizaji nyota wa Filamu nchini Elizabeth Michael a.k.a Lulu (17) anaehusishwa na kifo cha Muigizaji Mwenzie, Marehemu Steven Kanumba, aliye fariki dunia Aprili 7 mwaka huu nyumbani kwake maeneo ya Vatican Sinza Jijini Dar es Salaam. Akiwa katika muonekano mpya tokea amepelekwa lupango. Kwa sasa msanii huyu anaonekana kunenepa wakati kila mtu anaamini yuko kwenye kipindi kigumu sana pengine kuliko vipindi vyote katika maisha yake tangu azaliwe. Kingine najiulizaga siku zote ile mimba ambayo ilikua ikiongelewa sana imepotelea wapi?
Monday, September 10, 2012
NDOA YA MTITU YAGHARIMU 25 MIL
William Mtitu.
MSANII wa kiwanda cha filamu Bongo, William Mtitu anayetarajia kufunga ndoa Jumamosi ijayo, ametoa ripoti kuwa, bajeti ya harusi yake itakula kiasi cha Sh. milioni 25 za Kitanzania.
Akichezesha taya na paparazi wetu, jana Jumatano jijini Dar, Mtitu alisema mpaka sasa kamati ya harusi yake imefanikiwa kukusanya mkononi Sh. milioni 16 huku watu mbalimbali wakiendelea kuahidi na kutoa.
Alisema ndoa yake hiyo itakayofungwa katika katika Kanisa la Mtakatifu Joseph lililopo Posta, Dar, itafuatiwa na sherehe ya kukata na mundu kwenye Ukumbi wa Urafiki-Ubungo ambapo mavazi yatakayovaliwa na waalikwa ni ya kawaida.
SINTAH NI MENEJA MPYA WA CHIDY BEENZ
List ya managers wanaowasimamia wasanii wa bongo flava inazidi kuongezeka baada ya Sintah kutagaza kum-sign Chidy Beenz kuwa chini yake.
Hatujui deal hilo lina thamani ya kiasi gani lakini inaonekana kama Chidy ameamua kutumia experience aliyoko nayo Sintah pamoja na elimu yake ili ku-boost his public image na mziki wake pia.
‘Education is power and that is why Chidy kawaacha wote na kunitafuta mimi, sasa mambo ndo yameanza“, alihollarSintah ambapo Chidi Beenz chini ya usimamizi wake atafanya show ya kwanza at New Maisha Club on 30 September.
Aliongeza kuwa Chidi Benz will be dressed by Kidoti Fashion which is owned by Jokate ambaye ndiye anayewavalisha maceleb kibao kwa sasa hapa nchini.
SNURA AJUTA 'KUMDISS' WEMA
MUDA mchache umepita tangu msanii wa filamu bongo, Snura, kutangaza kuachana na rafiki yake kipenzi Wema Sepetu, sasa anaonekana kujirudi na kudai kuwa kuna vitu ameanza kuvimisi kutoka kwa mwanadada huyo ingawa anaona aibu kumuomba msahama na arudi tena kundini.
Mtandao huu ulimtafuta Snura kuzungumzia kwa ufupi kuhusiana na urafiki wake wa awali na Wema, ndipo alipofunguka kuwa vipo vingi na anaona haya kumuomba msamaha ili arundi tena kundini kwani anaamini akifanya hivyo watu watapata la kusema.
“Kuna vitu nimevimisi kuvifanya ambavyo nilikuwa nafanya pindi nilipokuwa na Wema, nilikuwa na hamu ya kuzungumza naye lakini naona kama nitawapa watu ncha kusema kitu ambacho sioni kama ni kizuri kwa wakati huu,” alidai.
Hata hivyo mtandao huo ulitaka kujua ni vitu gani alivyovimisi kutoka kwa Wema ambavyo yeye mweneywe hawezi kuvifanya, na alidai kuwa kutoka usiku na kuingia sehemu viwanja vikubwa vikubwa vya starehe ambazo huingia watu wazito ni moja ya kitu ambacho anahisi atavikosa kwa muda mrefu.
Mtandao huu ulimtafuta Snura kuzungumzia kwa ufupi kuhusiana na urafiki wake wa awali na Wema, ndipo alipofunguka kuwa vipo vingi na anaona haya kumuomba msamaha ili arundi tena kundini kwani anaamini akifanya hivyo watu watapata la kusema.
“Kuna vitu nimevimisi kuvifanya ambavyo nilikuwa nafanya pindi nilipokuwa na Wema, nilikuwa na hamu ya kuzungumza naye lakini naona kama nitawapa watu ncha kusema kitu ambacho sioni kama ni kizuri kwa wakati huu,” alidai.
Hata hivyo mtandao huo ulitaka kujua ni vitu gani alivyovimisi kutoka kwa Wema ambavyo yeye mweneywe hawezi kuvifanya, na alidai kuwa kutoka usiku na kuingia sehemu viwanja vikubwa vikubwa vya starehe ambazo huingia watu wazito ni moja ya kitu ambacho anahisi atavikosa kwa muda mrefu.
JACK WA CHUZI NA JINI KABULA WAFUMWA NDIVYO SIVYO
Kwa muda mrefu waigizaji wa kike wa Bongo Movies, Jack Pentzel na Miriam Jolwa aka Jini Kabula wamekuwa wakisakamwa na skendo ya usagaji kutokana na picha iliyosambaa kwenye mtandao inayowaonesha wakibusiana.
Hata hivyo wote wameendelea kukanusha kutojihusisha na vitendo hivyo kwa kudai kuwa walikuwa kazini.
Akiongena na kipindi cha Tagz Weekly cha DTV, Jack amesema hana uhusiano wowote wa kimapenzi na Miriam kwakuwa zile ni picha zilizochukuliwa wakati wakishoot movie.
“Mi mwenyewe nimezisikia kama wewe ulivyozisikia, lakini ukweli ni kwamba mimi ni msanii, ni msanii wa filamu nafanya kazi za kuelimisha jamii, kwamba jamii ntaifundisha kwamba ifanye hivi ntaikosoa ifanye hivi.
Kwahiyo zile ni picha ambazo zilipigwa wakati tupo location, na sio kwamba zile picha walizoziona wao ndio kile kitu sisi tulichokuwa tunakifanya. Sisi tulikuwa tunaigiza, hakuna uhalisia wowote wa kitu tulichokuwa tunakifanya”, alisema.
“Mimi nina mtu wangu, mimi nina mpenzi wangu, kwanza siwezi kuwa na mahusiano na mwanamke mwenzangu, kwasababu atanifanya nini mpaka mimi niridhike?”.Aliongeza
Kwa upande wake Miriam, naye alikanusha kuwa na uhusiano na mwanamke mwenzake na kusisitiza kile alichokisema mwenzie.
“Ni kweli hizo picha zipo, lakini sio kama namaanisha mimi na Jack Pentzel tulikuwa tunafanya huo uchafu. Hiyo ni movie tulikuwa tunacheza, mimi nilikuwa kama namuapproach Jack, yaani mimi ndio yule mwanamke msagaji halafu yeye ndio demu wangu. Na hiyo movie sijui kwanini inachelewa kutoka,” alisisitiza Miriam.
HEMED AND GELLY WA RHYMES NDANI YA TWO IDIOT
No doubt Comedy is nowadays doing good here in Tanzania.
Kufuatia hili singer wa “Ninachotaka“, “Alcohol” ambaye pia signs zake ziko kwenye movies za “Green Light” na “Crazy Love” is read to team up with Gelly wa Rhymes to do comedy.
Kufuatia hili singer wa “Ninachotaka“, “Alcohol” ambaye pia signs zake ziko kwenye movies za “Green Light” na “Crazy Love” is read to team up with Gelly wa Rhymes to do comedy.
Hemedy Suleiman aka Pretty Huge Dude, ambaye ni movie star ataungana na Gelly whose real name is George ambaye ni hit maker wa nyimbo za “Kikuku“, “I Love You” na “Barafu wa Moyo Wangu” kuingia location kwa ajili ya ku-shoot a their first romantic comedy movie to be called “Two Idiots“.
“Ni kweli mimi na PHD tuko tayari kufanya movie ya comedy ambayo roughly ita-cost seven million kuitengeneza chini ya E Media Company“- Gellywa Rhymes told BK.
Hemedy alipoulizwa utofauti wa movie hiyo yao ya comedy na comedy nyingine zilizopo hapa nchini this is what he said, “Wengi wamekuwa wakidhani kuwa comedy ni kukunya sura na kuanza kuigiza, but sisi tutatupia romantic issues na bado watu wacheke bila kulazimishwa“.
“Project hii haitaishia hapa kwani baada ya Two Idiots tuna mipango ya kuanza kuvuka borders na kwenda kutafuta comedians wa kimataifa ili kuipeleka sector hii anga a mbele zaidi“-Hemedy.
Sunday, September 2, 2012
"BONGO MOVIE IMENIFUNDISHA UHUNI. NILIPOKUWA KIJIJINI SIKUWA HIVI"....RECHO
MSANII anayetokea mkoani Ruvuma ambaye kwa sasa a ametengeneza jina kupitia tasnia ya filamu Rachel Haule ‘Recho’, amebainisha kuwa tasnia hiyo ndiyo iliyombandilisha kimavazi tofauti na alipokuwa anatoka kijijini kwao Songea.
Mwandishi wa mtandao huu alitaka kujua anazungumzia vipi juu ya skendo kadhaa zilizokuwa zinaelekezwa kwake kuwa anavaa mavazi ya kichokozi, ambapo alidai kuwa baada ya kuingia mjini kitambo kidogo alijikuta akitekwa na mji lakini alikuja kucharuka zaidi baada ya kuanza kujuana na wasanii wa bongo muvi ambao mara zote walimshauri kuvaa nguo fupi ili kuleta mvuto zaidi.
Aliongeza kuwa inawezekana yeye akajiona hana matatizo lakini kwa sababu tasnia hiyo ya bongo muvi inaonekana kuwa na matatizo mengi basi hata yeye watu wanamuona ana matatizo hayo ya watu wengine na hawezi kukataa kwa sababu tayari yupo kwenye chungu hicho kimoja.
“Si kwamba nilitaka kuharibiwa hapana yani nilijikuta tu napenda kuvaa mavazi ambao rafiki zangu wanavaa na kadri siku zilivyokuwa zinaenda nilizidi kuzoea” alisema.
Hata hivyo msanii huyo kwa upande wa filamu alidai kuwa zimeweza kumtangaza kwa namna moja ama nyingine na anaamini ataweza kufika mbali zaidi na kujitangaza kimataifa.
Source mpekuz
DUDE AKANA KUONEKANA KWA MGANGA TANGA
Kulwa Kikumba ‘Dude’.
STAA wa filamu za Bongo, Kulwa Kikumba ‘Dude’, hivi karibuni alionekana kwa mganga, Pangani Tanga ambako inadaiwa alikwenda kwa ajili ya kurejesha mali zake zilizoibwa.
Dude alipotafutwa kwa njia ya simu na kupatikana alikuwa na haya ya kusema:
“Mh! Nyie ni wambeya sana, mimi nimekuja Tanga kwa shughuli zangu za kikazi, hayo mengine ni kama ziada tu.”
JOKATE AMPONDA SNURA KWA KUJIFANYA MPAMBE WA WEMA SEPETU
MWANAMITINDO maarufu nchini Jokate Mwengelo, amedai kuwa msanii Snura asijifanye kuwa ameacha urafiki na best yake wa karibu Wema Sepetu kwani awali alikuwa kama mpambe ambaye alisahau kufanya kazi zake kwa kushindwa kusoma alama za nyakati.
Snura amefunguka hivi karibuni na kudai kuwa eti ameamua kuachana na Wema Sepetu kwa madai kuwa alikuwa anakosa muda wa kufanya kazi zake, na badala yake muda mwingi alikuwa akifanya biashara za Wema huku akiwa
kama amsimamizi, na kazi zake zikiwa hazifananikiwi na kusonga mbele.
Jokate alipotafutwa na mwandishi wa mtandao huu ili kutoa kauli yake juu ya Snura kuachana na best yake wa karibu Wema, alidai kuwa kikubwa alichoharibu Snura ni kujifanya mpambe kwani alishindwa kufanya ishu zake badala yake alijiona kama mpambe wa Wema kwa kumfuata kokote anapokuwa.
“Unajua Snura alikuwa kama mpambe wa Wema na alishindwa kusoma alama za nyakati na sasa anadai kuwa ameachana na Wema amepoteza muda kweli mi sioni kama atakuwa ni mkweli zaidi ya uongo alionao,” alidai.
Source: Vituko vya Mtaa
Snura amefunguka hivi karibuni na kudai kuwa eti ameamua kuachana na Wema Sepetu kwa madai kuwa alikuwa anakosa muda wa kufanya kazi zake, na badala yake muda mwingi alikuwa akifanya biashara za Wema huku akiwa
kama amsimamizi, na kazi zake zikiwa hazifananikiwi na kusonga mbele.
Jokate alipotafutwa na mwandishi wa mtandao huu ili kutoa kauli yake juu ya Snura kuachana na best yake wa karibu Wema, alidai kuwa kikubwa alichoharibu Snura ni kujifanya mpambe kwani alishindwa kufanya ishu zake badala yake alijiona kama mpambe wa Wema kwa kumfuata kokote anapokuwa.
“Unajua Snura alikuwa kama mpambe wa Wema na alishindwa kusoma alama za nyakati na sasa anadai kuwa ameachana na Wema amepoteza muda kweli mi sioni kama atakuwa ni mkweli zaidi ya uongo alionao,” alidai.
Source: Vituko vya Mtaa
Thursday, August 30, 2012
IMEVUJA SNURA AMWAGA UGALI, WEMA AMWAGA MBOGA
KUKIWA hakujapoa vizuri baada ya ushoga wao kuvunjika, mwigizaji wa sinema Bongo, Snura Mushi hivi karibuni alifanya mahojiano katika Runing a ya EATV, Kipindi cha Hot Mix ambapo alianza dalili za kumvua Miss Tanzania 2006 na staa wa sinema za Bongo, Wema Sepetu ambaye aliwahi kuwa shosti wake mkubwa.
Kwa mujibu wa macho ya mashuhuda, Snura alisisitiza kuwa, ana siri nzito za Wema na siku akiamua kuzianika, basi mrembo huyo hatakatiza mitaani kwa aibu.
Kwa maneno ya Snura, kila aliyetazama kipindi kile alisema hata kama mcheza filamu huyo hakuzitaja moja kwa moja siri za mwenzake, lakini kila mtu anajua Wema anatembea na aibu yake.
“Sasa kama Snura hakutaka kuzitaja hizo siri, kusema vile tu si tayari ameshamuumbua mwenzake, kila mtu anajua Wema ana mambo mabaya,” alisema Nice, mdada anayemiliki saluni moja iliyopo Kijitonyama, Dar.
Kama hiyo haitoshi, tayari Snura yupo kwenye mchakato wa kuandaa filamu inayoitwa Uozo wa Super Star ambayo ndani yake ni Wema mwanzo mwisho. Filamu hiyo inaandaliwa na Kampuni ya Chuz Entertainment ya Tuesday Kihangala ‘Chuz’.
Habari nyingine zinadai kuwa mara baada ya kumwagana na Wema, Snura kwa sasa amejipeleka kwa Chuz ambako ameigiza baadhi ya ‘sini’ kwenye Tamthiliya ya Jumba la Dhahabu ambayo inaingia mtaani hivi karibuni.
WEMA AMTAHADHARISHA SNURA
Wakati Snura akiwa na mengi ya moyoni, kwa upande wake, Wema alitoa msemo wa Wahenga akimwambia Snura, Kimya Kingi Kina Mshindo.
Alimtaka Snura anyamaze na afute nia yake kwani yeye akianza kuzungumza ya kwake anaamini Snura hataweza hata kutembea mitaani.
“Nayasikia mengi sana anayozungumza Snura lakini mi ni muungwana, asinione nipo kimya. Nikiamua kufunguka sitaweza kusikia la mnadi swala wala la muadhini.
“Hakuna mtu asiyejua kama mimi ndiye nilikuwa naendesha maisha yake kama mke wangu. Kila nguo nzuri anayoivaa kwa sasa au pochi anayobeba ni fedha zangu. Namuomba kabisa asinichokonoe,” alisema Wema.
Akaongeza: Nimeshamlipia kodi ya nyumba Snura, nimeshamsaidia kulipa ada ya mtoto wake, sasa ni kwa nini asiniheshimu?”
Wednesday, August 29, 2012
JENNIFER KYAKA [ODAMA] KUACHIA FILAMU MPYA - CHOCOLATE
Kampuni ya J-Film 4 Life chini ya Mkurugenzi Jennifer Kyaka (Odama) inapenda kukujuza kuwa mwezi Septemba 2012 itaachia filamu mpya ya Chocolate.
Mdau wangu naomba ukifika huo mwezi, wahi dukani na kununua filamu hii ambayo itakufanya uwe mtu wa tofauti kwa yale yaliyoigizwa. Tumekuelimisha, tumekufundisha, tumeadibisha na kukuburudisha.
J-Film 4 Life imehakikisha filamu ipo katika viwango vya kimataifa hasa sauti na video kwa ujumla.
Pata kuona hii trailer
J-Film 4 Life imehakikisha filamu ipo katika viwango vya kimataifa hasa sauti na video kwa ujumla.
Pata kuona hii trailer
Subscribe to
SIKU NILIYOKUWEPO KWA TB JOSHUA APRIL 2012
WATCH EMMANUEL TV LIVE-TB JOSHUA
Saturday, September 29, 2012
CHEMSHA BONGO NA BIBLE
MTUNZI: Rulea Sanga
ONYO: Tafadhali usiangalie majibu kabla ya kujibu kwa kutumia akilia yako
MASWALI
MASWALI
- (a) Kwanini Mafarisayo walitaka kumvizia Yesu katika Sinagogi kwa kutaka amponye mtu ambaye aliyepooza mkono wake wa kuume siku ya sabato.
(b) Baada ya Yesu kuona mawazo ya Mafarisayo kuhusu kumponya mtu aliyepooza mkono wake wa kuume, alimwambia nini kwa huyo aliyepooza
(c) Yesu aliwaambiaje Mafarisayo kuhusiana na alivyomponya mtu aliyepooza mkono wake wa kuume katikaSinagogi?
(d) Je, Yesu alimponya yule mtu aliyepooza mkono wake wa kuume? - Yesu aliporudi kutoka mlimani ambako alikuwa akioomba na kukesha usiku kucha, ni kwanini makutano walitaka kumgusa?
- Malizia misemo ya Bwana Yesu aliyosema kwa wanafunzi wake:
(a) Heri ninyi mlio na njaa-------------------------------------
(b) heri ninyi mliao sasa----------------------------------------
(c) Heri ninyi watu watakapowachukia na kuwatenga na kuwashutumu na kulitupa nje jina lenu kama neon ovu kwaajili ya Mwana wa Adam---------------------------------------------------
(d) Ole wenu mlio na mali, kwa kuwa--------------------------------------
(e) Ole wenu ninyi ambao mmeshiba sasa kwa kuwa-------------------------
(f) Ole wenu ninyi mnaocheka kwa kuwa------------------------------------- - Yesu alisemaje kwa wale ambao wanaotuchukia au adui zetu?
- Yesu anasema tufanye nini kwa wale
(a) Wanaotulaani
(b) Watupigao shavu moja
(c) Watunyang’anyao majoho yetu
(d) Watuombao
(e) Watunyang’anyao vitu vyetu
MAJIBU
- (a) Walitaka kumshitaki (Luka 6:7)
(b) Ondoka, simama katikati (Luka 6:8)
(c) Je, ni halali siku ya Sababto kutenda mema au kutenda mabaya; kuponya roho au kunyamaza? (Luka 6:9)
(d) Yesu aliwakaza macho, akawaambia, “Nyoosha mkono wako, akanyoosha mkono wake akawa mzima tena (Luka 6:10) - Kwasababu uweza ulikuwa ukimtoka ukiwaponya wote (Luka 6:19)
- (a) kwasababu mtashibishwa
(b) kwasababu mtacheka
(c)
(d) faraja yenu mmekwisha kuipata
(e) mtaona njaa
(f) mtabembelezwa
(Luka 6:20-26) - Tuwapende (Luka 6:27)
- (a) Tuwabariki (Luka 6:28)
(b) Tuwageuzie shavu la pili (Luka 6:29)
(c) Tusiwazuilie (Luka 6:29)
(d) Tuwape kile watuombacho (Luka 6:30)
(e) Tusitake waturudishie (Luka 6:30)
UFAHAMU WANGU NI MUHIMU KWAKO
UFAHAMU WANGU NI MUHIMU KWAKO ni kipengelee ambacho wewe mdau utakuwa unatoa mawazo yako juu ya swali ambalo tutakuwa tunakuuliza. Tutakurekodi katika kideo, ili watu waweze kukusikia LIVE ukichangia mawazo yako, ambayo RumAfrica inaamini yatakuwa msaada kwa watu wengine na wengi maisha yao ya kiimani yatabadilika.
Swali tutakalo anza nalo kwa sasa ni hili.
KWANINI MAKANISANI WATU WANAOKOKA SIKU ZA JUMAPILI NI WENGI SANA LAKINI KANISA HALIONGEZEKI?
Fredy Msungu ambaye ni mwimbaji wa nyimbo za injili Tanzania na mbeba maono ya "Pure Mission" alijaribu kufunguka na kueleza kile yeye anafahamu juu ya swali letu. Mazungomzo haya yalifanyika katika ofisi za RumAfrica sinza Afrikasana jijini Dar es Salaam.
Swali tutakalo anza nalo kwa sasa ni hili.
KWANINI MAKANISANI WATU WANAOKOKA SIKU ZA JUMAPILI NI WENGI SANA LAKINI KANISA HALIONGEZEKI?
Fredy Msungu ambaye ni mwimbaji wa nyimbo za injili Tanzania na mbeba maono ya "Pure Mission" alijaribu kufunguka na kueleza kile yeye anafahamu juu ya swali letu. Mazungomzo haya yalifanyika katika ofisi za RumAfrica sinza Afrikasana jijini Dar es Salaam.
UZINDUZI WA ALBAMU YA JANA IMEPITA YA MADAM RUTH NA CHRISS UMEFIKA SASA
Kama wewe ni mshabiki wa mambo ya MUNGU umefika wakati wa kushabikia kazi ya Mungu ambayo imefanywa kwa kupitia vinywa vya waimbaji wa injili Madam Ruth na Chriss. Kila siku tunasema ya kuwa Mungu ana njia nyingi za kuongea na walio wake, anaweza kuongea kwa kupitia watu au kiumbe chake chochote alichokiumba, leo hii anataka kuongea na wewe kwa njia ya uimbaji. Sasa ili uweze kumsikiliza huyu Mungu kwa kutokosa katika uzinduzi huu.
Watumishi wa Mungu wameamua kufanya uzinduzi huu bure ili ujumbe wa Mungu ukufikie hata wewe ambaye ungeshindwa kuwa na kiingilio, mtihani ulioko kwako ni kutafuta nauli yako ya kukuwezesha kufika katika kanisa la KKKT Ushirika wa Kariakoo hapa jijini Dar es Salaam.
Madam Ruth na Chriss wamenawa mikono mbele za Mungu wanasubiria kula chakula pamoja na wewe siku hiyo ya tarehe 28/10/2012 saa 8:00 mchana. Pia kuna waimbaji wengi sana watakuwepo kama unavyosoma katika tangazo hapo chini.
Tangazo hili limetengenezwa na
RumAfrica
Simu +255 715 851523
Blogu: www.rumafrica.blogspot.com
Barua Pepe: rumatz2011@yahoo.com
Thursday, September 27, 2012
BILA WACHUNGAJI NCHI HAINA PA KUKIMBILIA-KAMANDA KOVA
Huku likiendelea kulaumiwa kwa utendaji usiokidhi matumizi ya nguvu kupita kiasi, Jeshi la Polisi nchini limefungua na kueleza kuwa bila msaada wa watumishi wa Mungu juhudi zao za kukabiliana na uhalifu nchini hazitazaa matunda yoyote.
Akizungumza na chazo kimoja cha blog hii katika mahojiano maalumu wiki iliyopita, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, alisema nchi inaelekea katika hali ya hatari, hivyo wameamua kukutana na wachungaji ili washirikiane nao katika kuirejesha kwenye utulivu.
Akizungumza na chazo kimoja cha blog hii katika mahojiano maalumu wiki iliyopita, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, alisema nchi inaelekea katika hali ya hatari, hivyo wameamua kukutana na wachungaji ili washirikiane nao katika kuirejesha kwenye utulivu.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova |
“Tumeamua kuwashirikisha watumishi ili wamlilie Mungu wao aliye hai, awezekurejesha amani ambayo imeanza kuyumbayumba. Kweli bila hao nchi yetu hatujui itaelekea wapi, tunaimani kubwa kwamba wana kitu cha ziada juu ya nchi,” alisema Kamanda Kova.
Kamanda Kova aliweka wazi kuwa, kwa kutambua umuhimu wa watumishi wa Mungu aliye hai wiki iliyopita walilifanya kikao maalumu nao jijini hapa, ili kuwasihi wamsihi Kristo alikumbuke taifa la Tanzania na kulirejesha katika amani.
Mkuu huyo wa Jeshi la Polisi,aliweka bayana kuwa, lengo la kikao hicho na watumishi hao wa Mungu ni kupanga mikakati ya kufanya kazi pamoja kwa kile alichodai kuwa kwa nguvu pekee za Jeshi hilo, hakuna chochote kitakachowezekana na nchi inaweza kuwa katika matatizo makubwa.
“Lengo la Jeshi la Polisi, kukutana na wachungaji lilikuwa ni nzuri tu, unajua sisi tunafanya doria ya kuzuia uhalifu kwa njia ya mwili, lakini wachungaji wanafanya doria kwa njia ya rohoni, kwa hiyo wao wana nafasi kubwa ya kuleta mafanikio makubwa nakukomesha hali iliyopo katika taifa kwa sasa, ambayo siyo nzuri,” alisema Kamanda.
Sambamba na hilo, alisema watumishi wa Mungu wanauwezo mkubwa wa kuwafundisha watu maadili mema, kwa kuwa kauli yao katika jamii inasikilizwa zaidi.
“Lazima nchi iwe na amani kwa kutumia mbinu zozote, unafikiri ndugu mwandishi mambo yakiharibika tutakimbilia wapi, hakuna pa kukimbilia mambo yakiharibika katika taifa letu, kwa hiyo lazima tushirikiane na wachungaji kukomesha uhalifu,” alisema Kamanda Kova.
Kamanda Kova aliwataka watanzania kuacha tabia ya kuleta vurugu katika taifa, huku wakijichukulia sheria mkononi na kusababisha madhara makubwa katika taifa, hali inayopelekea mvurugano kutokea hata wananchi wasiokuwa na hatia kupoteza maisha.
Kadhalika anawasihi wachungaji kote nchini kuwa na uchungu na taifa hili, washirikiane na Jeshi hilo bega kwa bega kurejesha amani ya taifa ambalo ni mfano hata katika nchi mbalimbali duniani na likikifahamika kama kisiwa cha amani.
Aliongeza kuwa Jeshi la polisi lilikiri mbele ya wachungaji hao kuwa kutumia nguvu na risasi, si suluhu na haitakuwa njia ya kutatua tatizo bali ni kuongeza matatizo zaidi, hivyo likaomba ushirikiano kwa taasisi mbalimbali za kidini hapa nchini kukemea vitendo vibaya vinavyoweza kuliweka taifa pabaya
Source: Gospelvisiontz
MWIMBAJI WA JOYOUS CELEBRATION KUANDIKA HISTORIA WIKI IJAYO
Khaya Mthethwa akiwa jukwaa la Joyous Celebration. |
Kundi la Joyous Celebration la nchini Afrika ya kusini linatarajia kuandika historia nchini mwao endapo mwimbaji wao kijana Khaya Mthethwa aliyeingia kwenye top 2 ya shindano la Idols nchini humo atashinda shindano hilo na kuwa mweusi wa kwanza kushinda tangu kuanzishwa kwa shindano hilo nchini humo.
Mwimbaji huyo kutoka jimbo la Durban amefanikiwa kuingia Top 2 akipambana na mpinzani mwenzake mwenye asili ya kizungu aitwaye Melissa kutoka Port Elizabeth, ambapo upigaji kura kwa washindanaji hao walioweza kuwabwaga wenzao zaidi ya 30 hadi kufikia hapo, unaendelea kwa kuongezwa siku zaidi hadi jumatatu tarehe 1 mwezi 10, ambapo waimbaji hao watakuwa na nafasi ya kuimba hapo kesho katika ukumbi wa Mosaiek Teatro.
Kijana huyo ameonyesha kipaji kikubwa katika shindano hilo na kujikusanyia mashabiki wengi nchini humo ambao wamekuwa wakishirikiana na kundi la Joyous kufanya kampeni mbalimbali ili watu wapate kumpigia kura hatimaye kuibuka mshindi katika kinyang'anyiro hicho ambacho watu wengi(weusi) wanataka kumpigia kura Khaya ili ashinde na kuandika historia nchini humo.
Mwimbaji huyo kutoka jimbo la Durban amefanikiwa kuingia Top 2 akipambana na mpinzani mwenzake mwenye asili ya kizungu aitwaye Melissa kutoka Port Elizabeth, ambapo upigaji kura kwa washindanaji hao walioweza kuwabwaga wenzao zaidi ya 30 hadi kufikia hapo, unaendelea kwa kuongezwa siku zaidi hadi jumatatu tarehe 1 mwezi 10, ambapo waimbaji hao watakuwa na nafasi ya kuimba hapo kesho katika ukumbi wa Mosaiek Teatro.
Kijana huyo ameonyesha kipaji kikubwa katika shindano hilo na kujikusanyia mashabiki wengi nchini humo ambao wamekuwa wakishirikiana na kundi la Joyous kufanya kampeni mbalimbali ili watu wapate kumpigia kura hatimaye kuibuka mshindi katika kinyang'anyiro hicho ambacho watu wengi(weusi) wanataka kumpigia kura Khaya ili ashinde na kuandika historia nchini humo.
Wakati huo huo kundi lake la Joyous Celebration siku ya Jumamosi na Jumapili katika ukumbi wa Teatro Montecasino, linatarajiwa kugawa zawadi kwa mashabiki wake kwa kuimba nyimbo mpya na zazamani ikiwa pamoja na kuwaalika waimbaji waliowahi kuimbia katika kundi hilo awali ambao watapata kuwakumbusha wapenzi wao nyimbo walizowahi kuimba wakiwa na kundi hilo. Kati ya waimbaji ambao kuna uwezekano wakawepo katika onyesho hilo lililopewa jina la MTN Joyous Celebration Rewind, kuna Keke, Kgotso, Swazi,Pastor Patric Duncan, William Sejake, Nqubeko na mkewe Ntokozo na waimbaji wengine wengi.
Source:Gospel Kitaa
Source:Gospel Kitaa
You might also like:
RUMAFRICA YATEMBELEWA NA DR FADHILI EMILY WA THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC
Dk. Fadhili Emily ni mtumishi wa Mungu katika kanisa la Kisabato hapa jijini Dar es Salaam. Siku ya leo ametutembelea katika ofisi zetu Afrikasana Sinza hapa jijini Dar es Salaam kwa lengo la kutaka kutujuza dawa zake zinatokana na matunda na mimea. Dawa hizi zimekuwa msaada mkubwa sana kwa wale waliowahi kuzitumia. Pia Dk. Fadhili Emily alishauri watu kumuamini Mungu na kutambua mimea na matunda anayotumia ni uumbaji wa Mwenyezi Mungu.
Na haya ndio aliyoyataka tuyajue:
Dk Fadhili Emily
Ikiwa wewe umewahi kupimwa na ukajulikana kama una ugonjwa wako katika hospitali au zahanati zinazotambulika na serikali, basi waweza kutupigia simu katika namba +255 712 705158 au +255 757 931376, sisi tutakuunganisha na wakala (agents) wetu waliopo katika kila mkoa kwa kutumia mabsi na ndege kukufikishia huduma hii.
Na haya ndio aliyoyataka tuyajue:
Dk Fadhili Emily
THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC YAANZA KUTOA HUDUMA YA DAWA POPOTE PALE ULIPO
ZITAMBUE DALILI ZA HATARI ZA KIAFYA
- Upunguvu wa nguvu za kiume
- Tumbo kuunguruma wakati wa kuhisi njaa
- Kuwaka moto na ganzi mwilini
- Moyo kwenda mbio na pressure
- Kutoona siku za kike na kutokuwa na hamu ya mwanaume kwa wanawake
- kuwashwa na kutoka na uchafu nzito
- nnn
- Kuvimba miguu na ukibonueza linaachwa shimo
- Kuwashwa na kukosa usingizi
- kuvimba kwa korodani (mayai kwa wanaume wa ukiona mayai yako hayalingani
LISHE NA AFYA KWA WAATHILIKA WA VVU/UKIMWI TOKA THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC
Ugonjwa wa UKIMWI kisayansi ni kuathirika kwa uzaliwaji wa Cell Nyeupe za damu, ambazo husababisha upungufu wa kinga mwilini.
Mgonjwa wa UKIMWI kiafya ili asaidie uwiano wa cell zinazokutana na \ zinazozaliwa ni lazima ajitahidi kupata viini lishe muhimu ambavyo vinatoka katika chakula:
Mgonjwa wa UKIMWI kiafya ili asaidie uwiano wa cell zinazokutana na \ zinazozaliwa ni lazima ajitahidi kupata viini lishe muhimu ambavyo vinatoka katika chakula:
- Pendelea kutumia zabibu nyeusi (Black Current) kwa kuwa tunda hili lina sukari iliyochanganywa na uchafu asili kabisa ambao husaidia kuzalisha sukari ya sucrose ambayo huzalisha kwa wingi Cell Nyeupe za damu na kuongeza uwiano mzuri wa cell zinazokufa kwa kuzaliwa.
Zabibu na sucrose iliyosheheni vitamini C, Citric Acid na Acetic Acid na viini lishe vingi muhimu kwa CD4 na CD8. - Pendelea kutumia chai isiyotiwa majani ya chai.
· Katika chai yako weka majani ya mlonge yaliyokaushwa vyema na kusagwa.
· Chota kijiko cha chai cha unga wa majani hayo na weka katika kikombe kimoja cha chai,
· Katika maji ya moto usiweke sukari,
· Tia asali mbichi kabisa. Ni kifungua kinywa na kizuri haina uchungu wala harufu na
· Waweza kunywa na vitafunio vyako kama chai ya kawaida.
· Waweza kutumia mchana na jioni kwani chai hiyo inasaidia kusimamisha kasi ya kuzaliana kwa virusi na kuvifanya virusi vilivyopo kusinzia hivyo hautojisikia maumivu wala kupungua kwa kinga za mwili zinazohusika yaani CD4, hii ni kwasababu ya uwepo wa virutubisho cha Hydro Chloride katika mumea wa mronge (Drumstic).
Huu ni utafiti uliofanywa na THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha ROMALINDA UNIVERSITY OF MEDICINAL PLANT kilichoko California Marekani. Haina madhara yoyote, pia waweza kutembelea THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC iliyopo Mbezi Beach kupata dawa hiyo iliyoandaliwa tayari kwa viwango vya kidaktari kwa uasili wa hali ya juu sana.
Huu ni utafiti uliofanywa na THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha ROMALINDA UNIVERSITY OF MEDICINAL PLANT kilichoko California Marekani. Haina madhara yoyote, pia waweza kutembelea THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC iliyopo Mbezi Beach kupata dawa hiyo iliyoandaliwa tayari kwa viwango vya kidaktari kwa uasili wa hali ya juu sana.
- Pendelea kutumia vyakula vya mchanganyiko kama
- BAMIA + NYANYA CHUNGU + KAROTI + NYANYA MAJI + VITUNGUU + BINZARI + BILINGANYA.
- Chemsha vyote kwa pamoja visiive sana na
- Usiweke maji mengi sana. Ubichi wake (kijani) kwani chakula hicho ni kizuri kwa afya kwasababu ya uwepo wa Acaroids Acid ambayo pia inamsaada mkubwa wa kukinga maradhi nyemelezi.
- Tumia nafaka ambazo hazijakoborewa, mahindi, maharage, njugu mawe, njegere, mbaazi, dengu n.k hii huboresha viini lishe na kinga mwilini.
TUTEMBELELE THE FADHAGET SANITARIUM CLINIC TUPIME TUJUE CHANZO DAWA ZIPO
Wasiliana nasi kwa simu: +255 712 705158 | +255 757 931376 | +255 787 705158
Blogu: www.fadhaget.blogspot.com
Blogu: www.fadhaget.blogspot.com
Wednesday, September 26, 2012
KWANINI NATESEKA WAKATI YESU YUKO?
Kama wanadamu kuna mengi tunapitia katika maisha yetu,na kuna changamoto nyingi tunazipata katika mahangaiko ya kutafuta maisha bora. Kuna wengine maisha bora walishawapata lakini maisha yao ni ya mateso sana, pesa au mali zao zimekuwa hazina msaada katika maisha yao. Mungu haangalii sana mali zako wala pesa yako kukupa furaha na amani katika maisha yako. Tumeona watu wengi wanaishi katika majumba ya kifahari sana lakini hawana amani ndani ya mioyo yao, wasiwasi umetawala. Watu wa namna hii hawatamani hata kulala katika majumba yao kutokana na mateso wanayopata. Wengine ni wagonjwa sana na wamejaribu kwenda katika mahospitali makubwa kutibiwa lakini imeshindikana. Pesa zao zimekuwa hazina msaada kabisa. Kuna wengine wamejariwa kuwa na vyakula vya kila naman lakini kutokana na magonjwa yao wameambiwa baadhi ya vyakula wasile na wakila watakufa. Wengine wana magari ya kifahari sana lakini hawayatumii kutokana na magonjwa walionayo, na magari hayo yanatumika na watu wengine kabisa ambao hawakutoa jasho la kuyatafuta. Ki ukweli maisha yamekuwa hayaeleki kabisa.
Wewe unapolia unaumwa kichwa, wapo wanaokatwa miguu huko mahospitalini, wewe unapolia unaumwa malaria wapo wanaoondolewa macho na wanakuwa vipofu, wewe unapolia kuumwa tumbo wapo wanaokatwa mikono na kuwa vilema. Kwahiyo kila mtu anakilio chake.
Ndugu wamekuwa hawapendani katika familia zao, utaona ndugu yako wa damu anaamua kukuchezea kwa kukutupia majini au magonjwa ya ajabu. wengine wanathubutu kwenda kwa waganga kukuharibia maisha yako, na hii inatokana na wivu wa mamendeleo yako. Mapepo yanaanza kukusumbua na kukuabisha kwa kukuangusha mbele za watu, amani inatoweka kabisa. Ndugu yangu unayefanya mambo hayo ipo siku yatakurudia na utaabika.
Mimi sio wewe na wewe sio mimi, shida zangu sio shida zako na shida zako sio zangu, kucheka kwangu kwaweza kuwa kero kwako, na kero zako zaweza kuwa kicheko kwangu, kwahiyo tunatofautiana.
La msingi katika haya yote ni kutua mzigo wako kwa Yesu, na ukifanya hivyo huku ukimaanisha, ndugu yangu utafurahia hayo majumba yako, magari yako ya kifahari, magonjwa yako yatatoweka, amani katika maisha yako itatapakaa kila mahali. Unaweza kujiuliza kuwa utatuaje mizigo yako kwa Yesu:
Kwanza mkubali Yesu kuwa kiongozi wako na hakuna mwingine zaidi yake.
Pili, fanya yale ambayo Yesu anataka uyafanye kwa uaminifu.
Tatu, Maagizo ya Yesu utayapata kwa kusoma Biblia na sio kusoma tu, bali kuyatendea kazi.
Nne, Shirikiana na wenzako katika kujadili yale ambayo umeyasoma katika Biblia ili imani yako iwe juu
Tano, Kuwa na imani ya kutosha kwa kuamni kila kitu kilichoko katika Biblia na yaamini maombi unayoomba
Sita, Uwe mtu wa maombi sana, hata kama unapitia katika magumu ya aina gani wewe kazana na maombi.
Kwa leo ngoja niishie hapo, Munguakinipa uhai tena tutazungumza mengine.
Asante Sana kwa kupoteza muda wako na kusoma kile Mungu amenielekeza nikifanye kwako.
RUMA AFRICA KUDONDOSHA MZIGO MPYA
RumAfrica imetengeza Tshirts mpya zenye kumtukuza Yesu na kuipongeza Emmanuel TV ya TB Joshua.
Jipatie Tshirts hizi kwa bei nafuu sana
Zinapatika ofisini kwetu Afrikasana sinza nyuma ya soko la mbogamboga na matunda.
Unaweza kutupigia +255 715 851523 au kutuma B/Pepe rumatz2011@yahoo.com.
Nakuomba utuunge mkono kwa mambo ya kimwili na Mungu wangu akubariki.
MAZISHI YA KARDINALI RUGAMBWA YAZUA JIPYA
Hayati Kardinali Laurean Rugambwa enzi za uhai wake. |
Hatua hiyo imekuja siku chache baada ya wafanyabiashara katika manispaa ya Bukoba, kutengeneza fulana zenye nembo ya kanisa hilo na picha ya kardinali Rugambwa, ambazo zinauzwa kwa sh.12,000 bila ridhaa ya uongozi wa kanisa hilo.
Akizungumza na gazeti majira katibu wa kanisa katoliki jimbo la Bukoba, Padri Deodatus Rwehumbiza, alisema waumini ambao watanunua fulana zilizotengenezwa na wafanyabiashara hao bila baraka za kanisa hilo, watakuwa wamefanya makosa......
Limeandika Gazeti Majira.
*MAREHEMU AGNESS YAMO AAGWA LEO, KUZIKWA MOROGORO KESHO
Wanahabari, ndugu, jamaa na marafiki wakipita kwenye jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Mwandishi wa Habari wa gazeti la Tanzania Daima, Agness Christopher Yamo, na kutoa heshima zao za mwisho, wakati wa shughuli za kuaga mwili wa marehemu zilizofanyika leo mchana Buguruni, jijini Dar es Salaam, ambapo baada ya kuagwa marehemu alishafirishwa kuelekea mjini Morogoro kwa maziko.
Yamo alifariki dunia jana katika hospitali ya Jeshi, Lugalo, Dar es Salaam, alikokuwa amelazwa kwa matibabu. Mungu ailaze roho ya marehemu Agness mahala peponi, Amin.
Sehemu ya waandishi wa habari wanawake waliojitokeza katika msiba huo leo.
SHEREHE ZA KULITABARUKU KANISA KATOLIKI JIMBO LA BUKOBA MJINI BAADA YA UKARABATI MKUBWA ULIOCHUKUA MIAKA 17 KUFANYIKA 7/10/2012 NA MAZISHI YA MAREHEMU MWADHAMA KARDINAL RUGAMBWA NI 6/10/2012
Tarehe 7/10 /2012 kutafanyika sherehe za kulitabaruku Kanisa Katoliki Jimbo la Bukoba Mjini baada ya ukarabati mkubwa uliochukua miaka 17.Shughuli ya kuzikwa upya kwa masalia ya Marehemu Kardinali Rugambwa itakwenda sambamba na sherehe za kuadhimisha miaka 100 tangu kuzaliwa kwake.
Mwadhama Laurean Kardinali Rugambwa,aliyekuwa Kardinali wa kwanza Mtanzania na Mwafrika alifariki dunia 8/12/1997 na kuzikwa tarehe 17/12/1997 kwa muda katika Kanisa Katoliki lililopo Kashozi Wilaya ya Bukoba Vijijini kutokana na ukarabati uliokuwepo katika kanisa hili pichani na sasa unakamili ni Kanisa la Jimbo Katoliki Bukoba.
Marehemu Mwadhama Kardinali Laurean Rugambwa alizaliwa tarehe 12/7/1912 katika eneola Rutabo Kamachumu Wilaya ya Mulebwa na alikuwa Padri 12/12/1947 na aliteuliwa kuwa Kardinali 23/3/1960.
Shughuli hizi zinatarajiwa kuhudhuriwa na watu zaidi ya 10,000 kutoka nje ya Bukoba,viongozi mbalimbali pamoja na maaskofu kutoka Ulaya,Kenya,Uganda, Burundi, na mabalozi mbalimbali na viongozi wakuu wa nchi ni sehemu ya Waalikwa!!.
PURE MISSION KUWAWEKA VIJANA WA KIKRISTO KATIKA HALI YA KUJITAMBUA
Fredy Msungu siku ya leo alitembelea ofisi za Rumafrica kwaajili ya kutambulisha project yake na Angel Benard inayoitwa “Pure Mission”. Pia alisema kuna watu 15 waofanya nao kazi na wengine wako mikoni na vyuoni kama vile chuo cha Mzumbe Morogoro, Tumaini Iringa, UD na vingine vingi.
Alisema, lengo kuu la project kuwaweka vijana tayari katika kupambana na changamoto nyingi zinazowakabili vijana wa Kikristo Tanzania. Pure Mission inawalenga vijana wa kizazi kipya kuwa bora hasa kwa wale watakaoshika vitengo nyeti serikalini na makampuni ya watu binafsi
Vitu vinavyofanyika katika Pure Mission ni Talk Show, Movement mbalimbali kwa vijana, Praise and Worship, Motivation kwa vijana walioko mashuleni na vyuoni,
Fred alimshukuru Mungu kwa kuwawezesha kwa kazi hii ambayo wanayofanya kwaajili ya vijana.
Pure Mission huwa inafanya matamasha makubwa matatu kwa mwaka, mwanzoni mwa mwaka, katikati mwa mwaka na mwishoni mwa mwaka. Na sasa wako mwisho wa mwaka kwahiyo kuna tamasha limeandaliwa mkoani Iringa ambapo tarehe 19 Octoba 2012 watakuwa katika Chuo cha Tumaini, tarehe 20 Octoba watakuwa Chuo cha RUCO na tarehe 21 Octoba 2012 kutakuwa na Shout of Joy Concert ukumbi wa Highland Hall kuanzia saa 9:00 Mchana – 3:00 usiku.
Mengine mnaweza kusikiliza katika clip hiyo hapo chini, ni memgi yamezungumziwa:
Fred alimshukuru Mungu kwa kuwawezesha kwa kazi hii ambayo wanayofanya kwaajili ya vijana.
Pure Mission huwa inafanya matamasha makubwa matatu kwa mwaka, mwanzoni mwa mwaka, katikati mwa mwaka na mwishoni mwa mwaka. Na sasa wako mwisho wa mwaka kwahiyo kuna tamasha limeandaliwa mkoani Iringa ambapo tarehe 19 Octoba 2012 watakuwa katika Chuo cha Tumaini, tarehe 20 Octoba watakuwa Chuo cha RUCO na tarehe 21 Octoba 2012 kutakuwa na Shout of Joy Concert ukumbi wa Highland Hall kuanzia saa 9:00 Mchana – 3:00 usiku.
Mengine mnaweza kusikiliza katika clip hiyo hapo chini, ni memgi yamezungumziwa:
Fredy Msungu ndani ya ofisi za Rumafrica
Tuesday, September 25, 2012
MKESHA ULIOFANYIKA KATIKA KANISA LA FULL VICTORY GOSPEL CHURCH IJUMAA ILIYOPITA
Katika mkesha huu kulikuwa na sifa na kuabudu, maombezi na Nrno la Mungu. Pia kulikuwa na mafundisho ya ujasiliamali. Waumini walijifunza jinsi ya kutunza pesa na kujitambua kutoka kwa walimu wa ujasiliamali ambao ni Sam Sasali na Prosper, hawa ndio waliowalisha waumini wa kanisa hilo chakula cha ujasiliamali. Mwimbaji wa nyimbo za Injili Steven Wambura alihubiri na kutoa ushuhuda wake, na jinsi gani Mungu amefanya kumiliki Studio yake hapa jijini Dar es Salaam.
Ijumaa hii pia kutakuwa na mkesha katika kanisa hilo, kwahiyo kama ulikosa mkesha uliopita, unakaribishwa mkesha wa wiki hii.
Rumafrica ilibahatika kuhudhuria katika mkesha huu ili kujipatia muujiza kutoka kwa Mungu kwa kupitia watumishi wake. Tuone baadhi ya picha na Clips
Mwalimu wa Ujasiliamali, Sam Sasali
Waumini
Elice Wangwe ambaye ni mke wa mwimbaji wa nyimbo za Injili Lyanga akiwauliza baadhi ya maswali kwa waumini wa kanisa lake kuhusu masomo ya ujasiliamali yaliyotolewa na walimu wao
PICHA ZINGINE TUNAZIWEKA
PICHA ZINGINE TUNAZIWEKA
MCHUNGAJI MTIKILA ASHINDA KESI KWA MSAADA WA YESU
Mwenyekiti wa Chama cha Democratic Party (DP), Mchungaji Christopher Mtikila.
MWENYEKITI wa Chama cha Democratic Party (DP), Mchungaji Christopher Mtikila, ameshinda kesi ya uchochezi iliyokuwa inamkabili.
Inadaiwa kuwa Oktoba 21 mwaka jana katika maeneo ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Ilala, jijini Dar es Salaam Mchungaji Mtikila alitoa maneno ya uchochezi, dharau na kujenga chuki dhidi ya Serikali na Rais.
Inadaiwa kuwa Oktoba 21 mwaka jana katika maeneo ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Ilala, jijini Dar es Salaam Mchungaji Mtikila alitoa maneno ya uchochezi, dharau na kujenga chuki dhidi ya Serikali na Rais.
Akizungumza na mtandao wa Global Publishers baada ya kushinda kesi hiyo, Mtikila amesema “Ushindi huu niliutarajia maana hata asubuhi kabla ya kuja mahakamani niliongea na Yesu na sasa amenijibu”.
Mara baada ya kushinda kesi hiyo lilizuka timbwili lingine baada ya mtu mmoja kujitokeza akiwa na RB (Report Book) akimtuhumu Mchungaji Mtikila kuwa alimtishia kumuua na ni mwizi wa viwanja. Baada ya kutaka kukamatwa na polisi mmoja aliyekuwa na cheo cha Koplo, Mchungaji alikataa kwa madai kuwa yeye ni kiongozi wa kitaifa hivyo hawezi kukamatwa na polisi mwenye cheo cha Koplo, labda polisi mwenye cheo cha SSP (Senior Superintendent of Police). Kwa kauli hiyo polisi alishindwa kumtia nguvuni.
source: Strictly Gospel
MUIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI AGNESS HATUNAE TENA DUNIA.
Kwaya ya Uinjilisti Kanisa la KKKT Kariakoo,wanasikitika kutangaza msiba wa muimbaji mwenzao Bi Agnes Yamo, kilichotokea katikta hospital ya Lugalo asubuhi ya leo saa 2:30
Agnes alizaliwa mwaka 1978 na mwaka 2012 ndio mwisho wa ndoto zake za kuwepo duniani.
Taratibu zote za msiba mtajulishwa kwa kupitia vyombo mbalimbali na hasa blogu hii ikishirikiana na blogu ya Madam Ruth na Chriss (www.madamruti.blogspot.com).
Taratibu zote za msiba mtajulishwa kwa kupitia vyombo mbalimbali na hasa blogu hii ikishirikiana na blogu ya Madam Ruth na Chriss (www.madamruti.blogspot.com).
Bwana alito na Bwana ametwaa Jina lake libarikiwe..Amina.
Source: www.madamruti.blogspot.com
Monday, September 24, 2012
CHEMSHA BONGO NA BIBLE
Mtunzi: Rulea Sanga
ONYO: Ni dhambi kubwa sana kuona unaangalia majibu kabla ya kujibu kwa kutumia Bongo yako. Jitahidi kujibu kwa kutumia akilia yako kabla ya kuangalia jibu.
MASWALI
ONYO: Ni dhambi kubwa sana kuona unaangalia majibu kabla ya kujibu kwa kutumia Bongo yako. Jitahidi kujibu kwa kutumia akilia yako kabla ya kuangalia jibu.
MASWALI
- (a) Yesu aliingia kwenye chombo cha nani cha kuvulia samaki wakati wavuvi wakiwa wametoka kuosha nyavu zao?
(b) Je, Yesu alifundisha watu waliokuwa katika chombo cha wavuvi?
(c) Ni kitu gani Simoni Petro alikifanya kwa Yesu baada ya kuona samaki aliokuwa anavua wamejaa katika vyombo vyao viwili?
(d) Unafikiri Simoni Petro alishikwa na mshangao alipoona samaki ni wengi sana, yeye pamoja na Yakobo na Yohana?
(e) Yesu aliwaambia nini, Simon baada ya kushangazwa na wingi wa samaki ambao hakutegemea kuwavua? - (a) Mtu mwenye ukoma, alifanya nini ili alipomuona Yesu na aliomba nini kwa Yesu?
(b) Yesu alifanyaje kumponya mtu mwenye ukoma?
(c) Baada ya kutakasika mwenye ukoma, Yesu alimwambia nini cha kufanya kwa kuhani? - (a) Baada ya watu waliomchukua mtu mwenye kupooza kukosa nafasi kutokana na wingi wa watu waliokuwa wakimsikiliza Yesu. Walitumia njia gani kumfikia Yesu ili amponye?
(b) Yesu baada ya kuona imani ya waliombeba yule mwenye kupooza, aliwambia nini?
(c) Waandishi walisema nini baada ya kuona Yesu ametoa msamaha wa dhambi kwa yule aliyepooza?
(d) Yesu aliwaambia nini waadishi hao baada ya kuona mioyo yao?
(e) Watu walipomuona yule mwenye kupooza akijitwika kile alichokilalia, Je, watu hao ni kitu gani walikifanya? - (a) Taja jina la mtoza ushuru ambaye Yesu alikutana naye baada ya kumponya mwenye kupooza
(b) Yesu aliambiwa nini na huyo mtoza ushuru baada ya kuonana naye?
(c) Kwanini Mafarisayo walinung’unika walipomuona Yesu anakula chakula na kunywa pamoja na watoza ushuru?
(d) Karama ilifanywa na nani kuwakusanya mafarisayo, watoza ushuru na Yesu kula chakula na kunywa?
(e) Yesu aliwajibuje wale Mafarisayo waliokuwa wanashangaa kuona Yesu anakula na watoza ushuru? - Yesu alisema maneno haya baada ya kusikia nini kutoka kwa Mafarisayo, “Je, Mwaweza kuwafanya wafunge walioalikwa harusini, akiwapo Bwana harusi pamoja nao?” Lakini siku itakuja watakapoondolewa Bwana harusi ndipo watakapofunga siku zile
MAJIBU
- (a) Simoni (Luka 5:3)
(b) Ndiyo (Luka 5:4)
(c) Alianguka magotini pa Yesu akisema, “Ondoka kwangu kwa maana mimi ni mwenye dhambi, Bwana” (Luka 5:8)
(d) Ndiyo walishikwa na mshangao (Luka 5:9)
(e) “Usiogope, tangu sasa utakuwa ukivua watu” (Luka 5:10) - (a) Alianguka kifudifudi na akamuomba Yesu akisema, “Baba ukitaka waweza kunitakasa” (Luka 5:12)
(b) Aliunyosha mkono wake akamgusa akisema “Nataka takasika” (Luka 5:13)
(c) Nenda ukajionyeshe kwa kuhani ukatoe kwaajili ya kutakasika kwako kama Musa alivyoamuru, iwe ushuhuda kwao” (Luka 5:14) - (a) Walipanda juu ya dari wakampitisha katika matofali ya juu wakamshusha yeye na kitanda chake katikati mbele ya Yesu (Luka 5:19)
(b) Ee, rafiki umesamehewa dhambi zako (Luka 5:20)
(c) Walihojiana wakisema, “Ni nani huyu asemaye maneno ya kukufuru? Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake? (Luka 5:21)
(d) “Mnahojiana nini mioyoni mwenu? Kusema umesamehewa dhambi zako au kusema Ondoka, uende? Lakini mjue ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi. (Luka 5:22-23)
(e) Walishikwa na mshangao, wakamtukuza Mungu, wakajaa hofu, wakisema leo tumemuona mambo ya ajabu (Luka 5:25) - (a) Lawi (Luka 5:27)
(b) “Nifuate” (Luka 5:27)
(c) Kwasababu watoza ushuru walionekana kuwa wenye dhambi (Luka 5:30)
(d) Lawi (Luka 5:29)
(e) Wenye afya hawana haja ya tabibu, isipokuwa walio hawawezi, sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi wapate kutubu (Luka 5:31) - Baada ya kuona wanafunzi kufunga mara nyingi, na kuomba dua, kadharika wanafunzi wa Mafarisayo, lakini wanafunza wa Yesu kunywa na kula (Luka 5:32)
JAJI WARIOBA AWAASA WAKRISTO KUPENDANA
Mwenyekiti wa tume Tume ya Marekebisho ya Katiba, Jaji Joseph Warioba. |
“ Ni vyema sisi waumini wa Kikristo, tukaonyesha utaifa kwa kutekeleza kwa vitendo amri mbili kuu zilizotolewa na Yesu Kristo , ikiwemo ya kututaka tuwapende jirani zetu kama nafasi zetu. Tukifanya hivyo, tutaondokana na hii tabia imbayo imenza kujengeka hapa nchini; yaani ubinafsi” alisema Warioba mbaye alikuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi huo.
Aliwashauri Wakristo wawe mfano kwa kutii sheria za nchi na kwamba wasichezee amani kwani pia ni kinyume cha maandiko matakatifu ambayo yanasisitiza binadamu wote kupendana
BETRICE WA FOREVER LIVING PRODUCT AMKARIBISHA RAFIKI YAKE KANISANI KWANZA KABLA YA MAFUNDISHO YA FLP KUANZA
Rulea Sanga wa Ruma Africa, jana aliakwa katika mafundisho ya bidhaa za Forever Living Product katika ukumbi wa Mayr Fair jijini Dar es Salaam. Mkutano huu uliwakusanya watu mbalimbali, watumiaji na wauzaji wa bidhaa za FLP. Kulikuwa na kutiana moyo na kuonyesha faida za utumiaji wa bidhaa hizo. Watu waliofanikiwa katika biashara ya FLP walitoa njia walizozitumia mpaka sasa wa mamilionea.
Kitu kilichonifurahisha blogger wenu, ni pale mwenyeji wangu Betrice alipowambia kuwa hakuweza kufika katika mafundisho yaliyokuwa yanaendelea asubuhi ya Jumapili kwasababu alikuwa kanisani na mgeni wake kutoka Nigeria ambaye alimshawishi kujiunga na FLP, alisema rafiki yake huyo walikutana naye kanisani, kwahiyo na yeye aliona ni vizuri kwenda kanisani kwanza kabla ya kufika katika mafundisho ya FLP. Betrice alisema amefanikiwa sana na biashara ya FLP na kipato chake ni kikubwa ukifananisha alipokuwa akifanya kazi UK. Betrice professional ni Engineer.
Rulea katika mafundisho ya utumiaji na faida za FLP
Betrice kulia akielezea mafanikio aliyopata kwa kutumia bidhaa za FLP
Betrice kulia akielezea mafanikio aliyopata kwa kutumia bidhaa za FLP
MC na ni mmoja wa watu waliofanikiwa sana na biasha ya FLP
Betrice wa pili kutoka kulia akifanya mawasiliano
Wahudhuriaji
MC Luvanda aliyevalia miwani akiwa katika mawsiliano huku akipata vitu kutoka kwa wazungumzaji wa FLP
AFLEWO NAIROBI NI NEXT LEVEL
Kwa wale waliofatilia kwenye Mtandano wa ntv.com event ya Aflewo Nairobi Watakubaliana na Mimi kuwa Aflewo ni Next Level.
Siku Ya Ijumaa Ya Tarehe 21 August, 2012 Katika Jiji na la Nairobi, Big Event Ya Aflewo ilifanyika na kuhudhuriwa na Maelfu ya Watu.
Event hiyo ya AFLEWO (Africa Lets Worship) ambayo ilifanyika Dar-es-Salaam Mwanzoni Mwa Mwaka huu na Kisha katika jiji la Kigari Rwanda, Wiki Ijayo itafanyika katika Jiji La Mombasa.
Aflewo ni Usiku wa Kusifu na Kuabudu na Maombi.
Sehemu Ya Umati Wa Watu Waliohudhuria Aflewo Nairobi.
Wazee Wa Kazi The Voice From Tanzania Wakifanya mambo Jukwaani.
Watu Wakifurahia The Voice Jukwaani.
Aflewo Team Kutoka Tanzania Ikiwa Jukwaani
Mwenyekiti wa Aflewo Tanzania Geofrey Obiero akiwa ndani ya Aflewo Nairobi
Hii nahisi Ilikuwa Ruka Kimasai....John Kagaruki akiwa hewani na Pastor Safari Wakati wa Kuongoza Praise Ndani Ya Aflewo Nairobi.
Praise Team Ya Tanzania Wakiwa Jukwaani.
Kila Nikimuona John Kagaruku akiwa katika Muonekano Huu basi nakumbuka Sifa Zivume.
Mdada Huyu Mlemavu akiteta Jambo ndani ya Mkesha Wa Aflewo.
Obedi Kiongozi wa The Voice akaonesha One Love From Tanzania.
Ni Wakati Sasa wa Watanzania Ku Support Events zetu hasa Makampuni Ya Kikristo.
Watu wakipokea anointing
Twende Kazi
Dhuuu
The Praise Team
Watu Wakienda Sawa Usiku wa Aflewo
Bila Shaka Ayalikuwa mambo yetu Yaleeeeee
The Voice Wakienda Sawa.
Source: Sam Sasali
Siku Ya Ijumaa Ya Tarehe 21 August, 2012 Katika Jiji na la Nairobi, Big Event Ya Aflewo ilifanyika na kuhudhuriwa na Maelfu ya Watu.
Event hiyo ya AFLEWO (Africa Lets Worship) ambayo ilifanyika Dar-es-Salaam Mwanzoni Mwa Mwaka huu na Kisha katika jiji la Kigari Rwanda, Wiki Ijayo itafanyika katika Jiji La Mombasa.
Aflewo ni Usiku wa Kusifu na Kuabudu na Maombi.
Sehemu Ya Umati Wa Watu Waliohudhuria Aflewo Nairobi.
Wazee Wa Kazi The Voice From Tanzania Wakifanya mambo Jukwaani.
Watu Wakifurahia The Voice Jukwaani.
Aflewo Team Kutoka Tanzania Ikiwa Jukwaani
Mwenyekiti wa Aflewo Tanzania Geofrey Obiero akiwa ndani ya Aflewo Nairobi
Hii nahisi Ilikuwa Ruka Kimasai....John Kagaruki akiwa hewani na Pastor Safari Wakati wa Kuongoza Praise Ndani Ya Aflewo Nairobi.
Praise Team Ya Tanzania Wakiwa Jukwaani.
Kila Nikimuona John Kagaruku akiwa katika Muonekano Huu basi nakumbuka Sifa Zivume.
Mdada Huyu Mlemavu akiteta Jambo ndani ya Mkesha Wa Aflewo.
Obedi Kiongozi wa The Voice akaonesha One Love From Tanzania.
Ni Wakati Sasa wa Watanzania Ku Support Events zetu hasa Makampuni Ya Kikristo.
Watu wakipokea anointing
Twende Kazi
Dhuuu
The Praise Team
Watu Wakienda Sawa Usiku wa Aflewo
Bila Shaka Ayalikuwa mambo yetu Yaleeeeee
The Voice Wakienda Sawa.
Source: Sam Sasali
Subscribe to: Posts (Atom)