Ronaldo after being amazed by his own goal in Real Madrid's win over Deportivo La Coruna on Sept. 30.
Wednesday, October 3, 2012 12:59 PM
“MAISHA yetu ni kama kifaranga aliyekosa mama kwani hali zetu za
kiuchumi kila kukicha zinazidi kudhoofika kama mgonjwa wa
kwashiakoo’’,anasema Julius Machia ambaye ni kiongozi wa kikundi cha
umoja wa wafugaji wahamiaji bonde la Songwe lililopo wilayani Chunya
mkoani Mbeya.
Anabainisha kuwa endapo kiwango cha kupigwa faini ambazo sio halali kitaendelea ,mifugo yao itamalizika na watakuwa masikini na mzigo kwa serikali kwa kuwa wanaishi kwa kutegemea mifugo walionayo.
Machia anasema tangu zoezi la kukamata mifugo inayozidi 70 na kutozwa kwa kila mfugo unaozidi shilingi 20,000,kumesababisha matatizo mengi kwa wafugaji yakiwemo baadhi yao kuuwawa na askari kwa kupigwa risasi katika operesheni ya kamata mifugo na wafugaji kudhulumiwa kwa kupigwa faini kubwa hali ambayo inamlazimu mfugaji kuuza mifugo kwa bei ya hasara.
Hii ni risiti ambayo amepewa mfugaji baada ya kupigwa faini ya uharibifu wa mazingira ,hata hivyo mfugaji alitoa shilingi milioni sita ikiwa ni faini ya ng’ombe 300 sawa na kila mmoja shilingi 20,000,hata hivyo mtendaji ameandika shilingi 600,000 tu
“Kwa miaka 10 sasa zoezi la kukamata mifugo, limekuwa kama mvuta sigara huvuta sigara anapojisikia kiu kwa kuwa watendaji wa serikali wanaendesha zoezi hili bila mpangilio na limekuwa linafanyika mara kwa mara tena kwa unyanyasaji mkubwa’’,anasisitiza Machia. Julius Machia anasema faini wanayotozwa na serikali kwa kila mfugo unaozidi imekuwa inafanyika katika mazingira ya kifisadi kwa kuwa kiwango cha faini ni kikubwa na kwamba kinachoandikwa kwenye risiti za malipo ya Halmashauri ya wilaya na hali halisi ni tofauti.
Aliyetakiwa kupokea fedha hizo ni mkulima ambaye shamba lake limeliwa na mifugo kupitia ofisi za vijiji badala yake mpokeaji wa fedha hizo ni Afisa mifugo,kilimo na ushirika wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya ambaye amesaini katika risiti kuwa amepokea kiasi hicho cha fedha.
Risiti nyingine ya mwezi Mei mwaka 2011 inaonesha kuwa mfugaji Julius Machia wa kijiji cha Chang’ombe alilipa faini ya shilingi milioni sita kwa ajili ya kuzidi mifugo 300 ambapo kila mfugo uliozidi ulitozwa shilingi 20,000,hata hivyo risiti hiyo imeandikwa mfugaji huyo amelipa shilingi laki sita badala ya milioni sita.
“Tumepumzika kwa miezi sita,tu Mei 16 na Juni mosi mwaka huu afisa mifugo akiwa na viongozi wengine wamefika tena kwenye bonde letu safari hii wametoza faini ya uharibifu wa mazingira ng’ombe na mbuzi zinazozidi kila mfugo shilingi 20,000,wamekusanya mamilioni ya shilingi,tumewandikiwa risiti ambazo sio halali tunaomba serikali isikilize kilio chetu, anasema mfugaji Machia.
Wafugaji wahamiaji wengine waliopigwa faini ya kuzidi kwa mifugo na kuandikiwa risiti kuwa ni faini kwa ajili ya kulisha mifugo kwenye mashamba ni Misa Njigula wa kijiji cha Totowe ambaye alipigwa faini ya shilingi 1,275,000 kwa ajili ya ng’ombe 255,Masale Gidai wa kijiji cha Magamba alipigwa faini ya shilingi 770,000.
Kiongozi wa kikundi cha wafugaji bonde la Songwe Julius Machia
Masele Julius wa kijiji cha Ifuko alipigwa faini ya shilingi 140,000,Mashala Kwilasa wa kijiji cha Galula alipigwa faini ya shilingi 115,000 na mfugaji John Kasema wa Totowe ametozwa faini ya shilingi milioni nane kwa ng’ombe 400.
“Tanzania ni nchi inayosifika kuongoza kwa kufuata utawala wa sheria,sisi wafugaji wahamiaji tumechoka kunyanyaswa, kukandamizwa, kukamatwa ovyo,kutozwa faini zisizo za haki kwanini kama sisi ni wahalifu tusipelekwe mahakamani ili haki itendeke’’,anasema mfugaji Machia.
Sisi wafugaji tulio wengi hatujasoma,tunadhulumiwa mifugo yetu kwa miaka kumi sasa,wewe nenda ukaone maisha ya watumishi wa umma wakiwemo watendaji , madiwani pamoja na viongozi ngazi ya wilaya sisi wenye mifugo tunaonekana masikini,watumishi hao wametajirika kutokana na mifugo yetu’’,anadai Machia.
Asilimia 90 ya wafugaji wahamiaji katika Bonde la Songwe hawajui kusoma,kuandika na kuhesabu hali ambayo inawafanya baadhi ya watendaji serikalini kutumia mwanya huo kuwadhulumu kwa kuwapiga faini ambazo sio halali.
Hata hivyo afisa mifugo na kilimo katika Halmashauri ya wilaya ya Chunya Adamu Mbale amekiri kuwepo kwa baadhi ya watendaji kuhusika na utoaji wa risiti ambazo sio halali“Kuna watendaji wawili kutoka vijiji vya Bonde la Songwe ambao wamechunguzwa na TAKUKURU baada ya kubainika kufanya udanganyifu kwenye risiti za malipo na kesi zao zipo mahakamani’.
Deus Mashalla mfugaji katika kijiji cha Galula anasema kitendo cha kukamata mifugo ya wafugaji wahamiaji kimekuwa kinafanyika sio kwa kuangalia idadi ya mifugo inayozidi 70 badala yake hata wakikuta mfugaji mhamiaji katika eneo lake kuna ng’ombe mmoja hukamatwa na kupelekwa katika kituo cha polisi na kumtoza mfugaji huyo kiasi cha shilingi 20,000.
Hata hivyo Mashalla anabainisha kuwa wanaoendesha operesheni ya kukamata mifugo wamekuwa wanavamia hata katika nyumba za wafugaji wahamiaji na kuwanyang’anya mifugo na kuwatendea vitendo vinavyokwenda kinyume na haki za binadamu.
Anavitaja vitendo hivyo kuwa ni kutishiwa risasi hewani ili wenye mifugo wajifiche na kuogopa kuuwawa,kupiga nyumba risasi hadi kubomoa ambapo wametolewa mfano nyumba ya mfugaji Jikolela Mihambo wa kijiji cha Swela nyumba yake iliteketea kwa moto baada ya kupigwa kwa risasi.
Afisa mifugo na kilimo wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Adamu Mbale
Vitendo vingine ambavyo vinakiuka haki za binadamu ni kuporwa kwa fedha za wafugaji,mgambo na askari kuwakimbiza wafugaji kwa magari na kuwasababishia majeraha wakati wakijitahidi kukimbia ili kujiokoa.
Wafugaji wahamiaji hao wamebainisha zaidi kuwa wafugaji wa bonde la Songwe ndiyo jamii inayooongoza kwa kilimo kwa kuwa wanazalisha mazao mengi ya chakula kama vile mahindi,mpunga,mtama na viazi vitamu na kwamba wafugaji hawapati tatizo la njaa ukilinganisha na wakulima wenyeji ambao karibu kila mwaka wanapata tatizo la njaa.
Gamaya Bunga mfugaji katika kijiji cha Chang’ombe anasema utozwaji wa faini unaonekana kufanyika kwa upendeleo kwa kuwa wakulima wanaovunja sheria na kulima kwenye maeneo ambayo hayaruhusiwi kisheria kama vile kwenye vyanzo vya maji vya mto Songwe na ziwa Rukwa hawakamatwi.
Bonde la Songwe lenye kata za Galula, Mbuyuni, Totowe, Namkukwe na Khanga lina utajiri mkubwa wa mifugo inayomilikiwa na wafugaji wahamiaji kutoka wa mikoa ya Tabora ,Shinyanga, Mwanza, Singida na Kagera ambapo inakadiriwa kuna mifugo zaidi ya 727,230 hadi kufikia mwaka jana.
Takwimu ambazo zimetolewa na afisa mifugo,kilimo na ushirika katika Halmashauri ya wilaya ya Chunya Adamu Mbale zinaonesha kuwa kati ya mifugo hiyo ng’ombe ni 286,800, mbuzi 46,501, kondoo 24,803, nguruwe 11,223 na kuku wa kienyeji 357,903.
Mbale anabainisha kuwa Kutokana na uwepo wa mifugo mingi serikali mwaka 2002 ilitoa sheria ya Halmashauri ya wilaya ya Chunya kuhakikisha kila mfugaji katika bonde hilo awe na mifugo isiyozidi 70 na kwamba mfugaji atakayezidisha kiwango hicho cha mifugo anapigwa faini ya shilingi 20,000 kwa kila mfugo unaozidi.
Operesheni ya kukamata mifugo iliyozidi ilikuwa inafanyika tangu mwaka 2001 hadi 2010 katika Bonde la Songwe kwa kuhusisha wadau mbalimbali wakiwemo watendaji wa serikali, mgambo, na polisi, hata hivyo kuanzia mwaka jana mkuu wa wilaya ya Chunya Deodatus Kinawiro alipiga marufuku operesheni hiyo akitaka wafugaji kwanza wapewe elimu ya kutosha.
Mkuu wa wilaya ya Chunya Deodatus Kinawiro katika kukabiliana na uingizaji wa mifugo ametoa wito kwa wakuu wa wilaya tisa zinazopakana na wilaya yake wasitishe utoaji wa vibali vya kusafirishia mifugo hasa Ng’ombe wanaoingia wilayani humo.
Wilaya zilizofikia muafaka wa kutotoa vibali vya uingizaji na utoaji wa vibali vya mifugo ni pamoja na Chunya, Mbarali, Mbeya, Mbozi, Mpanda, Sumbawanga, Sikonge, Urambo na Manyoni.
Ufisadi Chunya unatishia ustawi wa wafugaji
June 3rd, 2012 | by Albano MideloAnabainisha kuwa endapo kiwango cha kupigwa faini ambazo sio halali kitaendelea ,mifugo yao itamalizika na watakuwa masikini na mzigo kwa serikali kwa kuwa wanaishi kwa kutegemea mifugo walionayo.
Machia anasema tangu zoezi la kukamata mifugo inayozidi 70 na kutozwa kwa kila mfugo unaozidi shilingi 20,000,kumesababisha matatizo mengi kwa wafugaji yakiwemo baadhi yao kuuwawa na askari kwa kupigwa risasi katika operesheni ya kamata mifugo na wafugaji kudhulumiwa kwa kupigwa faini kubwa hali ambayo inamlazimu mfugaji kuuza mifugo kwa bei ya hasara.
Hii ni risiti ambayo amepewa mfugaji baada ya kupigwa faini ya uharibifu wa mazingira ,hata hivyo mfugaji alitoa shilingi milioni sita ikiwa ni faini ya ng’ombe 300 sawa na kila mmoja shilingi 20,000,hata hivyo mtendaji ameandika shilingi 600,000 tu
“Kwa miaka 10 sasa zoezi la kukamata mifugo, limekuwa kama mvuta sigara huvuta sigara anapojisikia kiu kwa kuwa watendaji wa serikali wanaendesha zoezi hili bila mpangilio na limekuwa linafanyika mara kwa mara tena kwa unyanyasaji mkubwa’’,anasisitiza Machia. Julius Machia anasema faini wanayotozwa na serikali kwa kila mfugo unaozidi imekuwa inafanyika katika mazingira ya kifisadi kwa kuwa kiwango cha faini ni kikubwa na kwamba kinachoandikwa kwenye risiti za malipo ya Halmashauri ya wilaya na hali halisi ni tofauti.
Ngombe wa
wafugaji wahamiaji wakisubiri kuuzwa kwa bei ya hasara mnadani ili
kuweza kulipa faini ambazo wanatozwa na Halmashauri zikiwemo mazingira,
kulisha mashamba na faini nyingine.
Baadhi ya risiti ambazo gazeti hili imepata nakala zake zinaonesha
kuwa mfugaji Materemki Lugola wa kijiji cha Wanzani alilipa faini ya
shilingi milioni 4,740,000 mwaka 2001 kwa ajili ya mifugo 948 kula
katika mashamba ya wakulima.Aliyetakiwa kupokea fedha hizo ni mkulima ambaye shamba lake limeliwa na mifugo kupitia ofisi za vijiji badala yake mpokeaji wa fedha hizo ni Afisa mifugo,kilimo na ushirika wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya ambaye amesaini katika risiti kuwa amepokea kiasi hicho cha fedha.
Risiti nyingine ya mwezi Mei mwaka 2011 inaonesha kuwa mfugaji Julius Machia wa kijiji cha Chang’ombe alilipa faini ya shilingi milioni sita kwa ajili ya kuzidi mifugo 300 ambapo kila mfugo uliozidi ulitozwa shilingi 20,000,hata hivyo risiti hiyo imeandikwa mfugaji huyo amelipa shilingi laki sita badala ya milioni sita.
“Tumepumzika kwa miezi sita,tu Mei 16 na Juni mosi mwaka huu afisa mifugo akiwa na viongozi wengine wamefika tena kwenye bonde letu safari hii wametoza faini ya uharibifu wa mazingira ng’ombe na mbuzi zinazozidi kila mfugo shilingi 20,000,wamekusanya mamilioni ya shilingi,tumewandikiwa risiti ambazo sio halali tunaomba serikali isikilize kilio chetu, anasema mfugaji Machia.
Wafugaji wahamiaji wengine waliopigwa faini ya kuzidi kwa mifugo na kuandikiwa risiti kuwa ni faini kwa ajili ya kulisha mifugo kwenye mashamba ni Misa Njigula wa kijiji cha Totowe ambaye alipigwa faini ya shilingi 1,275,000 kwa ajili ya ng’ombe 255,Masale Gidai wa kijiji cha Magamba alipigwa faini ya shilingi 770,000.
Kiongozi wa kikundi cha wafugaji bonde la Songwe Julius Machia
Masele Julius wa kijiji cha Ifuko alipigwa faini ya shilingi 140,000,Mashala Kwilasa wa kijiji cha Galula alipigwa faini ya shilingi 115,000 na mfugaji John Kasema wa Totowe ametozwa faini ya shilingi milioni nane kwa ng’ombe 400.
“Tanzania ni nchi inayosifika kuongoza kwa kufuata utawala wa sheria,sisi wafugaji wahamiaji tumechoka kunyanyaswa, kukandamizwa, kukamatwa ovyo,kutozwa faini zisizo za haki kwanini kama sisi ni wahalifu tusipelekwe mahakamani ili haki itendeke’’,anasema mfugaji Machia.
Sisi wafugaji tulio wengi hatujasoma,tunadhulumiwa mifugo yetu kwa miaka kumi sasa,wewe nenda ukaone maisha ya watumishi wa umma wakiwemo watendaji , madiwani pamoja na viongozi ngazi ya wilaya sisi wenye mifugo tunaonekana masikini,watumishi hao wametajirika kutokana na mifugo yetu’’,anadai Machia.
Asilimia 90 ya wafugaji wahamiaji katika Bonde la Songwe hawajui kusoma,kuandika na kuhesabu hali ambayo inawafanya baadhi ya watendaji serikalini kutumia mwanya huo kuwadhulumu kwa kuwapiga faini ambazo sio halali.
Hata hivyo afisa mifugo na kilimo katika Halmashauri ya wilaya ya Chunya Adamu Mbale amekiri kuwepo kwa baadhi ya watendaji kuhusika na utoaji wa risiti ambazo sio halali“Kuna watendaji wawili kutoka vijiji vya Bonde la Songwe ambao wamechunguzwa na TAKUKURU baada ya kubainika kufanya udanganyifu kwenye risiti za malipo na kesi zao zipo mahakamani’.
Deus Mashalla mfugaji katika kijiji cha Galula anasema kitendo cha kukamata mifugo ya wafugaji wahamiaji kimekuwa kinafanyika sio kwa kuangalia idadi ya mifugo inayozidi 70 badala yake hata wakikuta mfugaji mhamiaji katika eneo lake kuna ng’ombe mmoja hukamatwa na kupelekwa katika kituo cha polisi na kumtoza mfugaji huyo kiasi cha shilingi 20,000.
Hata hivyo Mashalla anabainisha kuwa wanaoendesha operesheni ya kukamata mifugo wamekuwa wanavamia hata katika nyumba za wafugaji wahamiaji na kuwanyang’anya mifugo na kuwatendea vitendo vinavyokwenda kinyume na haki za binadamu.
Anavitaja vitendo hivyo kuwa ni kutishiwa risasi hewani ili wenye mifugo wajifiche na kuogopa kuuwawa,kupiga nyumba risasi hadi kubomoa ambapo wametolewa mfano nyumba ya mfugaji Jikolela Mihambo wa kijiji cha Swela nyumba yake iliteketea kwa moto baada ya kupigwa kwa risasi.
Afisa mifugo na kilimo wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Adamu Mbale
Vitendo vingine ambavyo vinakiuka haki za binadamu ni kuporwa kwa fedha za wafugaji,mgambo na askari kuwakimbiza wafugaji kwa magari na kuwasababishia majeraha wakati wakijitahidi kukimbia ili kujiokoa.
Wafugaji wahamiaji hao wamebainisha zaidi kuwa wafugaji wa bonde la Songwe ndiyo jamii inayooongoza kwa kilimo kwa kuwa wanazalisha mazao mengi ya chakula kama vile mahindi,mpunga,mtama na viazi vitamu na kwamba wafugaji hawapati tatizo la njaa ukilinganisha na wakulima wenyeji ambao karibu kila mwaka wanapata tatizo la njaa.
Gamaya Bunga mfugaji katika kijiji cha Chang’ombe anasema utozwaji wa faini unaonekana kufanyika kwa upendeleo kwa kuwa wakulima wanaovunja sheria na kulima kwenye maeneo ambayo hayaruhusiwi kisheria kama vile kwenye vyanzo vya maji vya mto Songwe na ziwa Rukwa hawakamatwi.
Bonde la Songwe lenye kata za Galula, Mbuyuni, Totowe, Namkukwe na Khanga lina utajiri mkubwa wa mifugo inayomilikiwa na wafugaji wahamiaji kutoka wa mikoa ya Tabora ,Shinyanga, Mwanza, Singida na Kagera ambapo inakadiriwa kuna mifugo zaidi ya 727,230 hadi kufikia mwaka jana.
Takwimu ambazo zimetolewa na afisa mifugo,kilimo na ushirika katika Halmashauri ya wilaya ya Chunya Adamu Mbale zinaonesha kuwa kati ya mifugo hiyo ng’ombe ni 286,800, mbuzi 46,501, kondoo 24,803, nguruwe 11,223 na kuku wa kienyeji 357,903.
Mbale anabainisha kuwa Kutokana na uwepo wa mifugo mingi serikali mwaka 2002 ilitoa sheria ya Halmashauri ya wilaya ya Chunya kuhakikisha kila mfugaji katika bonde hilo awe na mifugo isiyozidi 70 na kwamba mfugaji atakayezidisha kiwango hicho cha mifugo anapigwa faini ya shilingi 20,000 kwa kila mfugo unaozidi.
Operesheni ya kukamata mifugo iliyozidi ilikuwa inafanyika tangu mwaka 2001 hadi 2010 katika Bonde la Songwe kwa kuhusisha wadau mbalimbali wakiwemo watendaji wa serikali, mgambo, na polisi, hata hivyo kuanzia mwaka jana mkuu wa wilaya ya Chunya Deodatus Kinawiro alipiga marufuku operesheni hiyo akitaka wafugaji kwanza wapewe elimu ya kutosha.
Mkuu wa wilaya ya Chunya Deodatus Kinawiro katika kukabiliana na uingizaji wa mifugo ametoa wito kwa wakuu wa wilaya tisa zinazopakana na wilaya yake wasitishe utoaji wa vibali vya kusafirishia mifugo hasa Ng’ombe wanaoingia wilayani humo.
Wilaya zilizofikia muafaka wa kutotoa vibali vya uingizaji na utoaji wa vibali vya mifugo ni pamoja na Chunya, Mbarali, Mbeya, Mbozi, Mpanda, Sumbawanga, Sikonge, Urambo na Manyoni.
No comments:
Post a Comment